15 wala hata Herode, kwa maana amemrudisha kwetu; basi tazama, hakuna neno lo lote alilolitenda lipasalo kufa.
16 Kwa hiyo nitamrudi, kisha nitamfungua. [
17 Maana ilimlazimu kuwafungulia mfungwa mmoja wakati wa sikukuu.]
18 Wakapiga kelele wote pamoja, wakisema, Mwondoe huyu, utufungulie Baraba.
19 Naye ni mtu aliyetupwa gerezani kwa ajili ya fitina iliyotokea mjini, na kwa uuaji
20 Basi Pilato alisema nao mara ya pili, kwa vile alivyotaka kumfungua Yesu.
21 Lakini wakapiga kelele, wakisema, Msulibishe. Msulibishe.