2 Naye alipoitwa, Tertulo akaanza kumshitaki, akisema,Kwa kuwa mnapata amani nyingi chini yako, Feliki mtukufu, na kwa maangalizi yako mambo mabaya yanatengenezwa kwa ajili ya taifa hili,
3 basi tunayapokea kila wakati na kila mahali, kwa shukrani yote.
4 Lakini nisikuudhi zaidi, nakusihi utusikilize maneno machache kwa fadhili zako.
5 Kwa maana tumemwona mtu huyu mkorofi, mwanzilishi wa fitina katika Wayahudi wote duniani, tena ni kichwa cha madhehebu ya Wanazorayo.
6 Na tena alijaribu kulitia hekalu unajisi; tukamkamata; [tukataka kumhukumu kwa sheria yetu.
7 Lakini Lisia jemadari akafika akamwondoa mikononi mwetu kwa nguvu,
8 Akawaamuru wale waliomshitaki waje kwako.] Wewe mwenyewe kwa kumwuliza-uliza utaweza kupata habari ya mambo yale yote tunayomshitaki sisi.