1 Siku ile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume.
2 Watu watauwa wakamzika Stefano, wakamfanyia maombolezo makuu.
3 Sauli akaliharibu kanisa, akiingia kila nyumba, na kuwaburuta wanaume na wanawake na kuwatupa gerezani.
4 Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno.