6 Lakini tangu mwanzo wa kuumbwa ulimwengu, aliwafanya mume na mke.
7 Kwa sababu hiyo mtu atamwacha babaye na mamaye, ataambatana na mkewe;
8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
9 Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
10 Hata nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo.
11 Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;
12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.