8 na hao wawili watakuwa mwili mmoja; hata wamekuwa si wawili tena, bali mwili mmoja.
9 Basi alichokiunganisha Mungu, mwanadamu asikitenganishe.
10 Hata nyumbani tena wanafunzi wakamwuliza habari ya neno hilo.
11 Akawaambia, Kila mtu atakayemwacha mkewe na kuoa mwingine azini juu yake;
12 na mke, akimwacha mumewe na kuolewa na mtu mwingine, azini.
13 Basi wakamletea watoto wadogo ili awaguse; wanafunzi wake wakawakemea.
14 Ila Yesu alipoona alichukizwa sana, akawaambia, Waacheni watoto wadogo waje kwangu, msiwazuie; kwa maana watoto kama hawa ufalme wa Mungu ni wao.