3 Nao wakuu wa makuhani walikuwa wakimshitaki mambo mengi.
4 Pilato akamwuliza tena akisema, Hujibu neno? Tazama ni mambo mangapi wanayokushitaki!
5 Wala Yesu hakujibu neno tena, hata Pilato akastaajabu.
6 Basi wakati wa sikukuu huwafungulia mfungwa mmoja, wamwombaye.
7 Palikuwa na mtu aitwaye Baraba, amefungwa pamoja na watu waliofanya fitina, na kufanya uuaji katika fitina ile.
8 Makutano wakaja, wakaanza kuomba awafanyie kama vile alivyozoea.
9 Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?