3 Sikilizeni; Tazama, mpanzi alitoka kwenda kupanda;
4 ikawa alipokuwa akipanda, mbegu nyingine ilianguka kando ya njia, wakaja ndege wakaila.
5 Nyingine ikaanguka penye mwamba, pasipokuwa na udongo mwingi; mara ikaota kwa kuwa na udongo haba;
6 hata jua lilipozuka iliungua, na kwa kuwa haina mizizi ikanyauka.
7 Nyingine ikaanguka penye miiba; ile miiba ikamea ikaisonga, isizae matunda.
8 Nyingine zikaanguka penye udongo ulio mzuri, zikazaa matunda, zikimea na kukua, na kuzaa, moja thelathini, moja sitini, na moja mia.
9 Akasema, Aliye na masikio ya kusikilia, na asikie.