30 Akaenda zake nyumbani kwake, akamkuta yule kijana amelazwa kitandani, na yule pepo amekwisha kumtoka.
31 Akatoka tena katika mipaka ya Tiro, akapita katikati ya Sidoni, akaenda mpaka bahari ya Galilaya, kati ya mipaka ya Dekapoli.
32 Wakamletea kiziwi, naye ni mwenye utasi, wakamsihi amwekee mikono.
33 Akamtenga na mkutano faraghani, akatia vidole vyake masikioni mwake, akatema mate, akamgusa ulimi,
34 akatazama juu mbinguni, akaugua, akamwambia, Efatha, maana yake, Funguka.
35 Mara masikio yake yakafunguka, kifungo cha ulimi wake kikalegea, akasema vizuri.
36 Akawaonya wasimwambie mtu; lakini kadiri ya alivyozidi kuwaagiza, ndivyo walivyozidi kutangaza habari;