2 Nawahurumia mkutano kwa sababu yapata siku tatu wamekaa nami, wala hawana kitu cha kula;
3 nami nikiwaaga waende zao nyumbani kwao hali wanafunga, watazimia njiani; na baadhi yao wametoka mbali.
4 Wanafunzi wake wakamjibu, Je! Ataweza wapi mtu kuwashibisha hawa mikate hapa nyikani?
5 Akawauliza, Mnayo mikate mingapi? Wakasema, Saba,
6 Akawaagiza mkutano waketi chini; akaitwaa ile mikate saba, akashukuru, akaimega, akawapa wanafunzi wake wawaandikie; wakawaandikia mkutano.
7 Walikuwa na visamaki vichache; akavibarikia, akasema wawaandikie na hivyo pia.
8 Wakala, wakashiba, wakakusanya mabaki ya vipande vya mikate makanda saba.