3 Basi Daudi akawakusanya Israeli wote huko Yerusalemu, ili kulipandisha sanduku la BWANA, mpaka mahali pake alipoliwekea tayari.
4 Daudi akawakutanisha wana wa Haruni, na Walawi;
5 wa wana wa Kohathi; Urieli mkuu wao, na nduguze mia na ishirini;
6 wa wana wa Merari; Asaya mkuu wao, na nduguze mia mbili na ishirini;
7 wa wana wa Gershoni; Yoeli mkuu wao, na nduguze mia na thelathini;
8 wa wana wa Elsafani; Shemaya mkuu wao, na nduguze mia mbili;
9 wa wana wa Hebroni; Elieli mkuu wao, na nduguze themanini;