7 Na hesabu yao, pamoja na ndugu zao waliofundishwa kumwimbia BWANA, wote waliokuwa wastadi, walikuwa mia mbili na themanini na wanane.
8 Wakatupiwa kura ya ulinzi wao, sawasawa wote, mdogo kwa mkubwa, mwalimu kwa mwanafunzi.
9 Kura ya kwanza ikamtokea Yusufu, kwa Asafu; ya pili Gedalia; yeye na nduguze na wanawe, kumi na wawili;
10 ya tatu Zakuri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
11 ya nne Seri, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
12 ya tano Nethania, wanawe na nduguze, kumi na wawili;
13 ya sita Bukia, wanawe na nduguze, kumi na wawili;