50 Na hawa ndio wana wa Haruni; mwanawe huyo ni Eleazari, na mwanawe huyo ni Finehasi, na mwanawe huyo ni Abishua;
51 na mwanawe huyo ni Buki, na mwanawe huyo ni Uzi, na mwanawe huyo ni Serahia;
52 na mwanawe huyo ni Merayothi, na mwanawe huyo ni Amaria, na mwanawe huyo Ahitubu;
53 na mwanawe huyo ni Sadoki, na mwanawe huyo ni Ahimaasi.
54 Basi haya ndiyo makao yao, sawasawa na marago yao mipakani mwao; wana wa Haruni, katika jamaa za Wakohathi; kwani walikuwa na kura ya kwanza;
55 wakapewa Hebroni, katika nchi ya Yuda, na vijiji vyake vilivyouzunguka;
56 bali mashamba ya mji huo, na vijiji vyake, alipewa Kalebu, mwana wa Yefune.