63 Na wana wa Merari walipewa kwa kura miji kumi na miwili, sawasawa na jamaa zao, katika kabila ya Reubeni, na katika kabila ya Gadi, na katika kabila ya Zabuloni.
64 Na wana wa Israeli waliwapa Walawi miji hiyo pamoja na viunga vyake.
65 Tena wakawapa kwa kura miji hiyo iliyotajwa majina yake, katika kabila ya wana wa Yuda, na katika kabila ya wana wa Simeoni, na katika kabila ya wana wa Benyamini.
66 Na jamaa nyingine za wana wa Kohathi walikuwa na miji ya mipakani mwao katika kabila ya Efraimu.
67 Basi wakapewa miji ya kukimbilia, yaani, Shekemu pamoja na viunga vyake katika nchi ya milima milima ya Efraimu; na Gezeri pamoja na viunga vyake;
68 na Yokmeamu pamoja na viunga vyake, na Beth-horoni pamoja na viunga vyake;
69 na Aiyaloni pamoja na viunga vyake, na Gath-rimoni pamoja na viunga vyake;