1 Naye Benyamini akamzaa Bela, mzaliwa wake wa kwanza, na wa pili Ashbeli, na wa tatu Ahiramu;
2 na wa nne Noha, na wa tano Rafa.
3 Na Bela alikuwa na wana; Adari, na Gera, na Abihudi;
4 na Abishua, na Naamani, na Ahoa;
5 na Gera, na Shufamu, na Huramu.