10 na Yeusi, na Shakia, na Mirma. Hao ndio wanawe, wakuu wa mbari za baba zao.
11 Naye alikuwa amezaliwa na Hushimu, Abitubu, na Elpaali.
12 Na wana wa Elpaali; Eberi, na Mishamu, na Shemedi, ambaye ndiye aliyejenga Ono na Lodi, pamoja na vijiji vyake;
13 na Beria, na Shema, waliokuwa wakuu wa mbari za baba zao miongoni mwa wenyeji wa Aiyaloni, wale ambao waliwakimbiza wenyeji wa Gathi.
14 Na Ahio, na Ghashaki, na Yeremothi;
15 na Zebadia, na Aradi, na Ederi;
16 na Mikaeli, na Ishpa, na Yoha; walikuwa wana wa Beria.