38 Wana wa Pashuri, elfu moja mia mbili arobaini na saba.
39 Wana wa Harimu, elfu moja na kumi na saba.
40 Walawi; wana wa Yeshua, na wana wa Kadmieli wa wana wa Hodavia, sabini na wanne.
41 Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane.
42 Akina bawabu; wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu, wana wa Hatita, wana wa Shobai; jumla yao ni mia moja thelathini na kenda.
43 Wanethini; wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi;
44 wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni;