6 Wakati wa kutafuta, na wakati wa kupoteza;Wakati wa kuweka, na wakati wa kutupa;
7 Wakati wa kurarua, na wakati wa kushona;Wakati wa kunyamaza, na wakati wa kunena;
8 Wakati wa kupenda, na wakati wa kuchukia;Wakati wa vita, na wakati wa amani.
9 Je! Mtendaji anayo faida gani katika yale anayojishughulisha nayo?
10 Nimeiona taabu ambayo Mungu amewapa wanadamu, ili kutaabika ndani yake.
11 Kila kitu amekifanya kizuri kwa wakati wake; tena ameiweka hiyo milele ndani ya mioyo yao; ila kwa jinsi mwanadamu asivyoweza kuivumbua kazi ya Mungu anayoifanya, tangu mwanzo hata mwisho.
12 Mimi najua ya kwamba hakuna jema kwao kupita kufurahi, na kufanya mema maadamu wanaishi.