3 Mtu akizaa watoto mia, akaishi miaka mingi, nazo siku za maisha yake ni nyingi, lakini nafsi yake haikushiba mema; tena ikiwa, zaidi ya hayo, amekosa maziko; mimi nasema, Heri mimba iliyoharibika kuliko huyo;
4 yaani, hiyo huja katika ubatili, na huenda gizani, nalo jina lake limefunikwa giza;
5 tena, haikuliona jua wala kulifahamu; basi, hii imepata kustarehe kuliko yule;
6 naam, ajapoishi miaka elfu mara mbili, asijiburudishe kwa mema; je! Wote hawaendi mahali pamoja?
7 Kazi yote ya binadamu ni kwa kinywa chake,Walakini hata hivyo nafsi yake hashibi.
8 Kwa maana mwenye hekima hupata faida gani kuliko mpumbavu? Au maskini ana nini kuliko yeye ajuaye kwenda mbele ya walio hai?
9 Heri kuona kwa macho,Kuliko kutanga-tanga kwa tamaa.Hayo nayo ni ubatili, na kujilisha upepo.