28 Waimbaji wakakusanyika kutoka uwanda na viunga vya Yerusalemu, na kutoka vijiji vya Wanetofathi;
29 tena toka Beth-gilgali, na toka mashamba ya Geba na Azmawethi; kwa maana waimbaji hao walikuwa wamejijengea vijiji katika viunga vya Yerusalemu.
30 Makuhani na Walawi wakajitakasa, nao wakawatakasa watu, na malango, na ukuta.
31 Ndipo nikawapandisha wakuu wa Yuda juu ya ukuta, nikawaagiza mikutano mikubwa miwili ya hao walioshukuru, na kuandamana; mmoja uende kwa kuume ukutani kuliendea lango la jaa;
32 na baada yao wakaenda Hoshaya, na nusu ya wakuu wa Yuda,
33 na Azaria, na Ezra, na Meshulamu,
34 na Yuda, na Benyamini, na Shemaya, na Yeremia,