6 Ni nani huyu apandaye kutoka nyikani,Mfano wake ni nguzo za moshi;Afukizwa manemane na ubani,Na mavumbi ya manukato yote ya mchuuzi?
7 Tazama, ni machela yake Sulemani;Mashujaa sitini waizunguka,Wa mashujaa wa Israeli.
8 Wote wameshika upanga,Wamehitimu kupigana;Kila mtu anao upanga wake pajaniKwa hofu ya kamsa za usiku.
9 Mfalme Sulemani alijifanyizia machelaYa miti ya Lebanoni;
10 Nguzo zake alizifanyiza za fedha,Na mgongo wake wa dhahabu,Kiti chake kimepambwa urujuani,Gari lake limenakishiwa njumu,Hiba ya binti za Yerusalemu.