2 Sikieni haya, enyi wazee;Sikilizeni, enyi wenyeji wote wa nchi.Je! Mambo haya yamekuwako katika siku zenu,Au katika siku za baba zenu?
3 Waarifuni watoto wenu habari yake,Watoto wenu wakawaambie watoto wao,Na watoto wao wakakiambie kizazi kingine.
4 Yaliyosazwa na tunutu yameliwa na nzige; na yaliyosazwa na nzige yameliwa na parare; na yaliyosazwa na parare yameliwa na madumadu.
5 Levukeni, enyi walevi, mkalie;Pigeni yowe, ninyi nyote mnywao divai;Kwa sababu ya divai mpya;Maana umekatiliwa mbali na vinywa vyenu.
6 Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu,Lenye nguvu, tena halina hesabu;Meno yake ni kama meno ya simba,Naye ana magego ya simba mkubwa.
7 Ameuharibu mzabibu wangu; ameuvunja mtini wangu; ameyaambua magamba yake kabisa; ameuangusha chini; matawi yake yamefanywa kuwa meupe.
8 Ombolea kama mwanamwali avaaye maguniaKwa ajili ya mume wa ujana wake.