1 Basi, tukiwa wafanyakazi pamoja na Mungu, tunawasihi msikubali ile neema mliyopokea kutoka kwa Mungu ipotee bure.
2 Mungu asema hivi:“Wakati wa kufaa nimekusikiliza,wakati wa wokovu nikakusaidia.”Basi, sasa ndio wakati wa kufaa; sasa ndiyo siku ya wokovu!
3 Kusudi tusiwe na lawama yoyote katika utumishi wetu, hatupendi kumwekea mtu yeyote kizuizi chochote.
4 Badala yake, tunajionesha kuwa kweli watumishi wa Mungu kwa kila kitu: Kwa uvumilivu mwingi wakati wa mateso, shida na taabu.