28 Simeoni alimpokea mtoto Yesu mikononi mwake huku akimtukuza Mungu, akisema:
29 “Sasa Bwana, umetimiza ahadi yako,umruhusu mtumishi wako aende kwa amani.
30 Maana kwa macho yangu nimeuona wokovu ulioleta,
31 ambao umeutayarisha uonekane na watu wote:
32 Mwanga utakaowaangazia watu wa mataifa,na utukufu kwa watu wako Israeli.”
33 Baba yake Yesu na mama yake walikuwa wakistaajabia maneno aliyosema Simeoni juu ya mtoto.
34 Simeoni akawabariki, akamwambia Maria mama yake, “Mtoto huyu atakuwa sababu ya kupotea na kuokoka kwa watu wengi katika Israeli. Naye atakuwa ishara itakayopingwa na watu;