53 Nao wakamcheka kwa sababu walijua kwamba alikuwa amekufa.
54 Lakini Yesu akamshika mkono akasema, “Mtoto, amka!”
55 Roho yake ikamrudia, akaamka mara. Yesu akaamuru wampe chakula.
56 Wazazi wake walishangaa, lakini Yesu akawaamuru wasimwambie mtu yeyote hayo yaliyotendeka.