18 Eneo lenyewe lilikuwa na miji ya Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Remethi, En-ganimu, En-hada na Beth-pasesi.
22 Kadhalika, mpaka wao ulifika Tabori, Shahasuma, Beth-shemeshi na kuishia kwenye mto Yordani. Jumla ya miji waliyopewa ni kumi na sita pamoja na vijiji vyake.
23 Hizo ndizo sehemu zilizopewa koo za kabila la Isakari; miji hiyo pamoja na vijiji vyake.
24 Kura ya tano ilizipata koo za kabila la Asheri.