14 tena kama Kristo hakufufuka, basi, kuhubiri kwetu ni bure na imani yenu ni bure.
15 Naam, na sisi tumeonekana kuwa mashahidi wa uongo wa Mungu; kwa maana tulimshuhudia Mungu ya kuwa alimfufua Kristo, ambaye hakumfufua, ikiwa wafu hawafufuliwi.
16 Maana kama wafu hawafufuliwi, Kristo naye hakufufuka.
17 Na kama Kristo hakufufuka, imani yenu ni bure; mngalimo katika dhambi zenu.
18 Na hapo wao nao waliolala katika Kristo wamepotea.
19 Kama katika maisha haya tu tumemtumaini Kristo, sisi tu maskini kuliko watu wote.
20 Lakini sasa Kristo amefufuka katika wafu, limbuko lao waliolala.