2 Kwa maana ikiwa mimi si mtume kwa wengine, lakini ni mtume kwenu ninyi; kwa maana ninyi ndinyi muhuri ya utume wangu katika Bwana.
3 Hilo ndilo jawabu langu kwa wale wanaoniuliza.
4 Je! Hatuna uwezo wa kula na kunywa?
5 Hatuna uwezo kuchukua pamoja nasi mke aliye ndugu, kama wao mitume wengine, na ndugu wa Bwana, na Kefa?
6 Au je! Ni mimi peke yangu na Barnaba tusio na uwezo wa kutokufanya kazi?
7 Ni askari gani aendaye vitani wakati wo wote kwa gharama zake mwenyewe? Ni nani apandaye mizabibu asiyekula katika matunda yake? Au ni nani achungaye kundi, asiyekunywa katika maziwa ya kundi?
8 Je! Ninanena hayo kwa kibinadamu? Au torati nayo haisemi yayo hayo?