1 Basi mitume na ndugu waliokuwako katika Uyahudi wakapata habari ya kwamba watu wa Mataifa nao wamelipokea neno la Mungu.
2 Na Petro alipopanda kwenda Yerusalemu, wale walio wa tohara wakashindana naye,
3 wakisema, Uliingia kwa watu wasiotahiriwa ukala nao.
4 Petro akaanza kuwaeleza kwa taratibu, akasema,