19 Mwalimu, Musa alituandikia ya kwamba ndugu ya mtu akifa, akamwacha mkewe wala hana mtoto, ndugu yake amtwae yule mkewe akampatie ndugu yake mzao.
20 Basi kulikuwa na ndugu saba, wa kwanza akatwaa mke, akafa, asiache mzao.
21 Wa pili naye akamtwaa akafa, wala yeye hakuacha mzao. Na wa tatu kadhalika;
22 hata na wote saba, wasiache mzao. Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
23 Basi, katika kiyama atakuwa mke wa yupi katika hao? Maana wote saba walikuwa naye.
24 Yesu akajibu, akawaambia, Je! Hampotei kwa sababu hii, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu?
25 Kwa maana watakapofufuka katika wafu, hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika walioko mbinguni.