20 Hata wakiisha kumdhihaki, wakamvua lile vazi la rangi ya zambarau, wakamvika mavazi yake mwenyewe; wakamchukua nje ili wamsulibishe.
21 Wakamshurutisha mtu aliyekuwa akipita, akitoka mashamba, Simoni Mkirene, baba yao Iskanda na Rufo, ili auchukue msalaba wake.
22 Wakamleta mpaka mahali paitwapo Golgotha, yaani, Fuvu la kichwa.
23 Wakampa mvinyo iliyotiwa manemane, asiipokee.
24 Wakamsulibisha, wakagawa mavazi yake, wakayapigia kura kila mtu atwae nini.
25 Basi ilikuwa saa tatu, nao wakamsulibisha.
26 Palikuwa na anwani ya mashitaka yake iliyoandikwa juu, MFALME WA WAYAHUDI.