9 Pilato akawajibu, akisema, Je! Mnataka niwafungulie mfalme wa Wayahudi?
10 Kwa maana alitambua ya kuwa wakuu wa makuhani wamemtoa kwa husuda.
11 Lakini wakuu wa makuhani wakawataharakisha makutano, kwamba afadhali awafungulie Baraba.
12 Pilato akajibu tena akawaambia, Basi nimtendeje huyu mnayemnena kuwa ni mfalme wa Wayahudi?
13 Wakapiga kelele tena, Msulibishe.
14 Pilato akawaambia, Kwani, ni ubaya gani alioutenda? Wakazidi sana kupiga kelele, Msulibishe.
15 Pilato akipenda kuwaridhisha makutano, akawafungulia Baraba; akamtoa Yesu, baada ya kumpiga mijeledi, ili asulibiwe.