36 uwaage watu hawa, ili waende zao mashambani na vijijini kandokando, wakajinunulie chakula.
37 Akajibu, akawaambia, Wapeni ninyi chakula. Wakamwambia, Je! Twende tukanunue mikate ya dinari mia mbili ili tuwape kula?
38 Akawaambia, Mnayo mikate mingapi? Nendeni mkatazame. Walipokwisha kujua wakasema, Mitano, na samaki wawili.
39 Akawaagiza wawaketishe wote, vikao vikao, penye majani mabichi.
40 Wakaketi safu safu, hapa mia hapa hamsini.
41 Akaitwaa ile mikate mitano na wale samaki wawili, akatazama mbinguni, akashukuru, akaimega ile mikate, akawapa wanafunzi wake wawaandikie; na wale samaki wawili akawagawia wote.
42 Wakala wote wakashiba.