48 Akawaona wakitaabika kwa kuvuta makasia, kwa maana upepo ulikuwa wa mbisho; hata ilipopata kama zamu ya nne ya usiku akawaendea, akitembea juu ya bahari; akataka kuwapita.
49 Nao walipomwona anatembea juu ya bahari, walidhani ya kuwa ni kivuli, wakapiga yowe,
50 kwa kuwa wote walimwona, wakafadhaika. Mara akasema nao, akawaambia, Changamkeni; ni mimi, msiogope.
51 Akapanda mle chomboni walimo; upepo ukakoma; wakashangaa sana mioyoni mwao;
52 kwa maana hawakufahamu habari za ile mikate, lakini mioyo yao ilikuwa mizito.
53 Hata walipokwisha kuvuka, walifika nchi ya Genesareti, wakatia nanga.
54 Nao wakiisha kutoka mashuani, mara watu walimtambua,