17 Basi utuambie, Waonaje? Ni halali kumpa Kaisari kodi, ama sivyo?
18 Lakini Yesu akaufahamu uovu wao, akasema, Mbona mnanijaribu, enyi wanafiki?
19 Nionyesheni fedha ya kodi. Nao wakamletea dinari.
20 Akawaambia, Ni ya nani sanamu hii, na anwani hii?
21 Wakamwambia, Ni ya Kaisari. Akawaambia, Basi, mlipeni Kaisari yaliyo ya Kaisari, na Mungu yaliyo ya Mungu.
22 Waliposikia, walistaajabu, wakamwacha, wakaenda zao.
23 Siku ile Masadukayo, watu wasemao ya kwamba hakuna kiyama, wakamwendea, wakamwuliza,