Mt.
Sura 22:24-30
Swahili Union Version
24wakisema, Mwalimu, Musa alisema, Mtu akifa, akiwa hana watoto, ndugu yake na amwoe yule mkewe, ili ampatie nduguye mzao.
25Basi, kwetu kulikuwa na ndugu saba; wa kwanza akaoa, akafariki, na kwa kuwa hana mzao, akamwachia nduguye mke wake.
26Vivyo hivyo wa pili naye, na wa tatu, hata wote saba.
27Mwisho wa wote yule mwanamke akafa naye.
28Basi, katika kiyama, atakuwa mke wa yupi katika wale saba? Maana wote walikuwa naye.
29Yesu akajibu, akawaambia, Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.
30Kwa maana katika kiyama hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika mbinguni.