Mt.
Sura 22:36-42
Swahili Union Version
36Mwalimu, katika torati ni amri ipi iliyo kuu?
37Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
38Hii ndiyo amri iliyo kuu, tena ni ya kwanza.
39Na ya pili yafanana nayo, nayo ni hii, Mpende jirani yako kama nafsi yako.
40Katika amri hizi mbili hutegemea torati yote na manabii.
41 Na Mafarisayo walipokusanyika, Yesu aliwauliza, akisema, Mwaonaje katika habari za Kristo?
42Ni mwana wa nani? Wakamwambia, Ni wa Daudi.