Mt.
Sura 25:17-23
Swahili Union Version
17Vile vile na yule mwenye mbili, yeye naye akachuma nyingine mbili faida.
18Lakini yule aliyepokea moja alikwenda akafukua chini, akaificha fedha ya bwana wake.
19Baada ya siku nyingi akaja bwana wa watumwa wale, akafanya hesabu nao.
20Akaja yule aliyepokea talanta tano, akaleta talanta nyingine tano, akisema, Bwana, uliweka kwangu talanta tano; tazama, talanta nyingine tano nilizopata faida.
21Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.
22Akaja na yule aliyepokea talanta mbili, akasema, Bwana, uliweka kwangu talanta mbili; tazama, talanta nyingine mbili nilizopata faida.
23Bwana wake akamwambia, Vema, mtumwa mwema na mwaminifu; ulikuwa mwaminifu kwa machache, nitakuweka juu ya mengi; ingia katika furaha ya bwana wako.