Mt.
Sura 25:5-11
Swahili Union Version
5Hata bwana arusi alipokawia, wote wakasinzia wakalala usingizi.
6Lakini usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, bwana arusi; tokeni mwende kumlaki.
7Mara wakaondoka wanawali wale wote, wakazitengeneza taa zao.
8Wale wapumbavu wakawaambia wenye busara, Tupeni mafuta yenu kidogo; maana taa zetu zinazimika.
9Lakini wale wenye busara wakawajibu, wakisema, Sivyo; hayatatutosha sisi na ninyi; afadhali shikeni njia mwende kwa wauzao, mkajinunulie.
10Na hao walipokuwa wakienda kununua, bwana arusi akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye arusini; mlango ukafungwa.
11Halafu wakaja na wale wanawali wengine, wakasema, Bwana, Bwana, utufungulie.