1 Ikawa Yesu alipomaliza maneno hayo yote, aliwaambia wanafunzi wake,
2 Mnajua ya kuwa baada ya siku mbili itakuwa Pasaka, na Mwana wa Adamu atasalitiwa asulibiwe.
3 Wakati ule wakuu wa makuhani, na wazee wa watu, wakakusanyika katika behewa ya Kuhani Mkuu, jina lake Kayafa;
4 wakafanya shauri pamoja, ili wamkamate Yesu kwa hila na kumwua.
5 Lakini wakasema, Isiwe wakati wa sikukuu, isije ikatokea ghasia katika watu.
6 Naye Yesu alipokuwapo Bethania katika nyumba ya Simoni mkoma,