Mt.
Sura 27:6-12
Swahili Union Version
6Wakuu wa makuhani wakavitwaa vile vipande vya fedha, wakasema, Si halali kuviweka katika sanduku ya sadaka, kwa kuwa ni kima cha damu.
7Wakafanya shauri, wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi liwe mahali pa kuzika wageni.
8Kwa hiyo konde lile huitwa konde la damu hata leo.
9Ndipo likatimia neno lililonenwa na nabii Yeremia, akisema, Wakavitwaa vipande thelathini vya fedha, kima chake aliyetiwa kima, ambaye baadhi ya Waisraeli walimtia kima;
10wakavitumia kwa kununua konde la mfinyanzi, kama Bwana alivyoniagiza.
11 Naye Yesu akasimama mbele ya liwali; liwali akamwuliza, akasema, Wewe ndiwe mfalme wa Wayahudi? Yesu akamwambia, Wewe wasema.
12Lakini aliposhitakiwa na wakuu wa makuhani na wazee, hakujibu hata neno.