1 Naye alipowaona makutano, alipanda mlimani; na alipokwisha kuketi, wanafunzi wake walimjia;
2 akafumbua kinywa chake, akawafundisha, akisema,
3 Heri walio maskini wa roho;Maana ufalme wa mbinguni ni wao.
4 Heri wenye huzuni;Maana hao watafarijika.
5 Heri wenye upole;Maana hao watairithi nchi.
6 Heri wenye njaa na kiu ya haki;Maana hao watashibishwa.