21 Mwingine katika wanafunzi wake akamwambia, Bwana, nipe ruhusa kwanza, niende nikamzike baba yangu.
22 Lakini Yesu akamwambia, Nifuate; waache wafu wazike wafu wao.
23 Akapanda chomboni, wanafunzi wake wakamfuata.
24 Kukawa msukosuko mkuu baharini, hata chombo kikafunikizwa na mawimbi; naye alikuwa amelala usingizi.
25 Wanafunzi wake wakamwendea, wakamwamsha, wakisema, Bwana, tuokoe, tunaangamia.
26 Akawaambia, Mbona mmekuwa waoga, enyi wa imani haba? Mara akaondoka, akazikemea pepo na bahari; kukawa shwari kuu.
27 Wale watu wakamaka wakisema, Huyu ni mtu wa namna gani hata pepo na bahari zamtii?