1 Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao.
2 Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
3 Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.
4 Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu?