Mt.
Sura 9:27-33
Swahili Union Version
27Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Mwana wa Daudi.
28Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana.
29Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate.
30Macho yao yakafumbuka. Naye Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema, Angalieni hata mtu mmoja asijue.
31Lakini wakatoka, wakaeneza habari zake katika nchi ile yote.
32Hata hao walipokuwa wakitoka, tazama, walimletea mtu bubu mwenye pepo.
33Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena, makutano wakastajabu, wakasema, Haijaonekana hivi katika Israeli wakati wo wote.