52 na mwanawe huyo ni Merayothi, na mwanawe huyo ni Amaria, na mwanawe huyo Ahitubu;
53 na mwanawe huyo ni Sadoki, na mwanawe huyo ni Ahimaasi.
54 Basi haya ndiyo makao yao, sawasawa na marago yao mipakani mwao; wana wa Haruni, katika jamaa za Wakohathi; kwani walikuwa na kura ya kwanza;
55 wakapewa Hebroni, katika nchi ya Yuda, na vijiji vyake vilivyouzunguka;
56 bali mashamba ya mji huo, na vijiji vyake, alipewa Kalebu, mwana wa Yefune.
57 Na wana wa Haruni wakapewa miji ile ya kukimbilia, nayo ni Hebroni, tena Libna pamoja na viunga vyake, na Yatiri, na Eshtemoa pamoja na viunga vyake;
58 na Holoni pamoja na viunga vyake, na Debiri pamoja na viunga vyake;