11 Pamoja na hayo, hao wana wa Kora hawakufa.
12 Na wana wa Simeoni kwa jamaa zao; wa Yemueli, jamaa ya Wayemueli; wa Yamini, jamaa ya Wayamini; na Yakini, jamaa ya Wayakini;
13 wa Sohari, jamaa ya Wasohari; wa Shauli, jamaa ya Washauli.
14 Hizi ndizo jamaa za Wasimeoni, watu ishirini na mbili elfu na mia mbili.
15 Na wana wa Gadi kwa jamaa zao; wa Sifoni, jamaa ya Wasifoni; wa Hagi, jamaa ya Wahagi; wa Shuni, jamaa ya Washuni;
16 wa Ezboni, jamaa ya Waezboni; wa Eri, jamaa ya Waeri;
17 wa Arodi, jamaa ya Waarodi; wa Areli, jamaa ya Waareli.