14 Hizi ndizo jamaa za Wasimeoni, watu ishirini na mbili elfu na mia mbili.
15 Na wana wa Gadi kwa jamaa zao; wa Sifoni, jamaa ya Wasifoni; wa Hagi, jamaa ya Wahagi; wa Shuni, jamaa ya Washuni;
16 wa Ezboni, jamaa ya Waezboni; wa Eri, jamaa ya Waeri;
17 wa Arodi, jamaa ya Waarodi; wa Areli, jamaa ya Waareli.
18 Hizi ndizo jamaa za wana wa Gadi kama waliohesabiwa kwao, arobaini elfu na mia tano.
19 Na wana wa Yuda, Eri na Onani; na hao Eri na Onani wakafa katika nchi ya Kanaani.
20 Na wana wa Yuda kwa jamaa zao; wa Shela, jamaa ya Washela; wa Peresi, jamaa ya Waperesi; wa Zera, jamaa ya Wazera.