42 Wakasafiri kutoka Salmona, wakapanga Punoni.
43 Wakasafiri kutoka Punoni, wakapanga Obothi.
44 Wakasafiri kutoka Obothi, wakapanga Iye-abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Wakasafiri kutoka Iye-abarimu, wakapanga Dibon-gadi.
46 Wakasafiri kutoka Dibon-gadi, wakapanga Almon-diblathaimu.
47 Wakasafiri kutoka Almon-diblathaimu, wakapanga katika milima ya Abarimu, kukabili Nebo.
48 Wakasafiri kutoka hiyo milima ya Abarimu, wakapanga katika nchi tambarare za Moabu, karibu na mto wa Yordani, hapo Yeriko.