16 Kisha BWANA akanena na Musa, na kumwambia,
17 Haya ndiyo majina ya watu watakaowagawanyia nchi iwe urithi wenu; Eleazari kuhani, na Yoshua mwana wa Nuni.
18 Kisha mtamtwaa mkuu mmoja wa kila kabila, ili waigawanye nchi iwe urithi wenu.
19 Na majina ya watu hao ni haya; katika kabila ya Yuda, ni Kalebu mwana wa Yefune.
20 Na katika kabila ya wana wa Simeoni, Shemueli mwana wa Amihudi.
21 Katika kabila ya Benyamini, ni Elidadi mwana wa Kisloni.
22 Na katika kabila ya wana wa Dani, mkuu, Buki mwana wa Yogli.