23 Nena na Haruni na wanawe, uwaambie, Hivi ndivyo mtakavyowabarikia wana wa Israeli; mtawaambia;
24 BWANA akubarikie, na kukulinda;
25 BWANA akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili;
26 BWANA akuinulie uso wake, na kukupa amani.
27 Ndivyo watakavyoweka jina langu juu ya wana wa Israeli; nami nitawabarikia.